Online Library TheLib.net » Mikidadi wa Mafia. Maisha ya Mwanaharakati na Familia Yake Nchini Tanzania
cover of the book Mikidadi wa Mafia. Maisha ya Mwanaharakati na Familia Yake Nchini Tanzania

Ebook: Mikidadi wa Mafia. Maisha ya Mwanaharakati na Familia Yake Nchini Tanzania

00
12.02.2024
0
0
Wazo la kuandika kitabu hiki limetokana na uhusiano wangu na kisiwa cha Mafia Tanzania, ulioanza takriban miaka arobaini na tano iliyopita. Katika muda huo nimetembelea Mafia mara saba na nimeandika na kuchapisha makala na vitabu vingi. Baadhi ya watu wanaoishi kisiwani wamekuwa rafiki zangu wa karibu; kiasi wamekuwa kama ndugu na nimeshiriki kwa karibu katika maisha yao.

Mmoja wao ambaye nilimjua vizuri tangu kukutana kwetu mwaka 1965 akiwa kijana mdogo ni Mikidadi Kichange. Huyu alinichukulia kama dada yake kwa miaka yote ya urafiki wetu hadi kifo kilipomchukua mapema mno mwaka 2002. Pamoja na mikutano yetu nilipokuwa nikienda Tanzania, alinifahamisha mengi kuhusu maisha yake kwa kuniandikia barua. Alinieleza juu ya elimu yake, mafunzo yake ya elimu ya misitu, Jeshi la Kujenga Taifa, ndoa yake na kuzaliwa kwa binti zake wawili; alivyokuwa akilea watoto wengi wa ndugu zake, kazi yake na alivyoanzisha shirika lisilo la serikali (NGO) ili kuboresha hali kisiwani. Ingawa Mikidadi hakufanikiwa kukamilisha elimu yake alivyotaka, alisoma vitabu vingi vya Kiswahili, Kiingereza na Kiarabu. Wakati tunakutana mara ya mwisho mwaka 2002 na kufanya kazi pamoja kule Mafia kwa miezi michache, alikuwa tayari ni mshirika wangu kikazi na pia ‘mdogo wangu’ na rafiki yangu.

Tangu kifo chake cha ghafla mwaka 2002 alipokuwa na umri wa miaka arobaini na tisa tu, nimetafakari jinsi anavyoweza kukumbukwa kwa kuandika kitabu kuhusu maisha yake, na kuonyesha mabadiliko makubwa yaliyotokea kisiwani Mafia na nchini Tanzania kwa jumla tangu ipate uhuru. Kitabu hiki ni wasifu wa kihistoria kwa upande mmoja na historia kwa kupitia wasifu kwa upande mwingine, ambamo maisha ya watu wa kawaida yanaonesha mapambano yao na maisha, changamoto, na katika mfano huu uwezo wa ajabu walio nao wa kuyashinda yote yanayowakabili.
Download the book Mikidadi wa Mafia. Maisha ya Mwanaharakati na Familia Yake Nchini Tanzania for free or read online
Read Download
Continue reading on any device:
QR code
Last viewed books
Related books
Comments (0)
reload, if the code cannot be seen